KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Monday, May 11, 2015

DAR MODERN TAARAB KUFANYA ZIARA MIKOA SITA


KIKUNDI cha taarab cha Dar Modern, kinatarajia kufana ziara katika mikoa sita nchini kwa lengo la kutambulisha ujio wake mpya katika muziki huo.

Ziara hiyo, iliyopewa jina la Modenika na Dar Modern,  italifikisha kundi hilo katika mikoa ya Rukwa, Katavi, Dodoma, Morogoro na Dar.

Mratibu wa ziara hiyo, Emmanuel Simon, alisema wiki hii kuwa, ziara hiyo itaanzia mkoani Mbeya, ambako kundi hilo litafanyika onyesho lake la kwanza Mei 20 mwaka huu katika mji mdogo wa Kyela.

Mei 22, mwaka huu, kundi hilo litafanya onyesho lingine katika mji mdogo wa Mpanda ulioko mkoani Katavi, wakati siku inayofuata, litahanikiza maraha katika mji wa Sumbawanga ulioko mkoani Rukwa.

Kwa mujibu wa Emmauel, baada ya maonyesho hayo, kundi hilo litarejea Dar es Salaam, ambako Mei 29, litafanya onyesho kwenye ukumbi wa Travertine ulioko Magomeni.

Mei 30, kundi hilo litakuwa kwenye ukumbi wa Royal Village ulioko mjini Dodoma na siku inayofuata, litamaliza ziara yake hiyo mjini Kilosa mkoani Morogoro kwa kufanya onyesho kwenye ukumbi wa Babylon.

Emmanuel amewataka mashabiki wa taarab kujitokeza kwa wingi kushuhudia maonyesho hayo, ikiwa ni pamoja na ujio mpya wa kundi hilo kwa vile limewaandalia mambo mazuri.

No comments:

Post a Comment