KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Friday, December 26, 2014

OGOPA KOPA WAJA NA TATU KALI MPYA


KUNDI jipya la muziki wa taarab la Ogopa Kopa, linaloongozwa na Malkia wa muziki huo nchini, Khadija Omar Kopa, limedhihirisha kuwa ni tishio baada ya kuibuka na vibao vipya  vitatu.

Moja ya vibao hivyo vipya ni Stop Red Card, kilichoimbwa na Anifa Maulid, almaarufu kwa jina la Jike la Chui, mwanadada mwenye sauti murua inayoleta starahamu ya aina yake masikioni.

Kibao kingine ni Chozi la mnyonge, kilichoimbwa na kijana anayechipukia katika muziki huo, Hassan Ali, ambaye amejaliwa kuwa na sauti maridhawa.

Kiongozi wa kundi hilo, Khadija Omar Kopa, naye ameibuka na kibao kikali kinachotarajiwa kubeba jina la albamu mpya ya kundi hilo, Mama mukubwa.

No comments:

Post a Comment