KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Tuesday, April 1, 2014

SUNGURA MJANJA WA MASHAUZI ATOA KITU KIPYA


MWIMBAJI chipukizi wa tarab anayeinukia vizuri nchini, Saida Ramadhani ‘Sungura Mjanja’, ameibuka na wimbo mpya uitwao Ropokeni Yanayowahusu.

Akizungumza na BIN ZUBEIRY jioni hii katika hoteli ya Double Tree, Masaki, Dar es Salaam, mwimbaji huyo wa kundi la Mashauzi amesema wimbo huo ametungiwa na dada yake, Isha Ramadhani.
“Dada Isha katunga, mimi nimerekodi na umekwishakamilika, ni wimbo mzuri sana, naamini utapendwa ukitoka. Na utazidi kunipandisha matawi ya juu,”alisema Saida.
Saida ameingia kwenye kinyang’anyiro cha tuzo za Kili mwaka huu kupitia wimbo wa Asiyekujua Hakuthamini, ambao ameshirikiana na dada yake, Isha ulioingia kwenye kipengele cha wimbo bora wa Taarab.

No comments:

Post a Comment