KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Tuesday, April 1, 2014

ISHA MASHAUZI AIBUKA NA SURA SIYO ROHO



MWANAMUZIKI na kiongozi wa kundi la taarab la Mashauzi Classic, Isha Mashauzi, ametoa nyimbo mpya mbili, ambazo muda si mrefu zitaanza kusikika kwenye vituo mbalimbali vya Redio nchini.
Akizungumza na BIN ZUBEIRY jioni hii katika hoteli ya Double Tree, Masaki, Dar es Salaam wakati wa semina ya wanamuziki waliongia kwenye tuzo za Kili 2014, Isha au Jike la Simba amesema kwamba nyimbo zote ni nzuri.
Amezitaja nyimbo hizo kuwa ni Sura Siyo Roho na Mapenzi Hayana Dhamana, ambazo zote ametunga yeye mwenyewe.
“Kama kawaida, wapenzi na mashabiki wangu na mashabiki wa Mashauzi Classic kwa ujumla, wajiandae kwa kazi mpya, tutaanza na audio (sauti) baadaye itafuatia na kwenye video pia,”alisema Isha.

No comments:

Post a Comment