KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Sunday, September 23, 2012

KHADIJA KOPA AMTUNGIA WIMBO MUMEWE

Mwimbaji nyota wa taarab nchini, Khadija Kopa akiwa na mumewe kabla ya kupanda stejini katika moja ya maonyesho yake.
Khadija Omar Kopa akilishambulia jukwaa akiwa sanjari na mabinti zake

Mwimbaji nyota wa taarab nchini, Khadija Omar Kopa ameibuka na kibao kipya kinachokwenda kwa jina la Nampenda mume wangu.
Kibao hicho alichokiimba kwa tashtiti ya hali ya juu kimeshaanza kutikisa anga za muziki kwa kupigwa mara kwa mara kwenye vituo mbalimbali vya redioni nchini.
Katika kibao hicho, Khadija anaelezea umuhimu wa wanawake kuwapenda na kuwaheshimu waume ama wapenzi wao badala ya kuwakashifu.
Anasema yeye binafsi anampenda mumewe na kumpatia kila anachokihitaji na kwamba katu hawezi kumuhini chochote.

No comments:

Post a Comment