KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Saturday, August 11, 2012

FELLA AFYATUA ALBAMU YA TAARAB


KIONGOZI wa kundi la muziki wa kizazi kipya la TMK Wanaume Family, Saidi Fella amesema yupo katika hatua za mwisho za kukamilisha albamu yake ya muziki wa taarab.
Akizungumza mjini Dar es Salaam wiki hii, Fella alisema tayari amesharekodi nyimbo tano za muziki na yupo katika maandalizi ya kuzindua albamu hiyo.
Fella alisema hadi sasa bado hajaipa jina albamu hiyo na kwamba amerekodi nyimbo zake akiwa na bendi yake ya Mkubwa na Wanawe, aliyoianzisha hivi karibuni.
“Ninachokifanya kwa sasa ni kuandaa maonyesho, ambayo nitaimba nyimbo hizo nikiwa na bendi yangu,”alisema kiongozi huyo na mwasisi wa TMK Wanaume Family.
Fella alisema ameamua kushika kipaza sauti na kuimba kwa lengo la kuongeza ujuzi wake baada ya kufanya vizuri katika muziki wa kizazi kipya.
Mkongwe huyo alisema baada ya uzinduzi wa albamu yake, atakuwa tayari kupanda jukwaa moja na kikundi chochote cha muziki huo kwa lengo la kufanya maonyesho ya pamoja.
“Cha msingi ni kujadili tu mambo ya maslahi, nikiridhika nitaimba,”alisema.
Kwa mujibu wa Fella, katika albamu yake hiyo mpya, amewashirikisha baadhi ya waimbaji nyota wa muziki huo kama vile Hassan Kumbi, Maua Tego, Isha Ramadhani ‘Mashauzi’ na Khadija Omar Kopa.

No comments:

Post a Comment