KWA HABARI ZA MUZIKI WA TAARAB, WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL ramozaone@gmail.com

Tuesday, August 21, 2012

CHID BENZ AMPA SHAVU KHADIJA KOPA


Kitu kimoja kizuri sana kumhusu Chidi Benz ni jinsi anavyoweza kuthubutu. Msanii anapoweza kuthubutu ina maana kwamba anakua katika sanaa yake na ni sehemu ya ubunifu.
Kama utakumbuka,siku za nyuma kidogo Chidi aliwahi kuthubutu kukutanisha Hip Hop/Bongo Fleva na muziki wa pwani katika kibao Mashaalaah alichoshirikiana vyema na Mzee Yusuph. Mambo yakaenda swadakta.Mashalaah ni mojawapo ya track nzuri mpaka hivi leo.
Katika muendelezo huo huo, hapa Chidi Benz anamshirikisha Malikia wa Mipasho,Bi.Khadija Omar Kopa.Wimbo unaitwa Nampenda Sana.

No comments:

Post a Comment